KWA HABARI NA UCHAMBUZI WA UHAKIKA,KITAIFA NA KIMATAIFA,USIKOSE KUTEMBELEA BLOG HII.

Friday, August 14, 2015

CHIMBUKO LA VYAMA VINGI NDANI YA MFUMO WA KIDEMOKRASIA

CHIMBUKO LA VYAMA VINGI NDANI YA MFUMO WA KIDEMOKRASIA

Na Farijala malid

Bismillah-Ar-rahaman

Kikawaida kwa kila zama,fikira katika ulimwengu ina chimbuko lake  ima chimbuko  hilo litoke kwa mwenyezi mungu  au kwa mwanadamu.Takribani miaka 100;{karne moja} katika umma huu waliishi nje ya fikira ambayo chimbiko lake ni Mwenyezi Mungu yaani mfumo wa Uislam ambao umeletwa kwa njia ya wahyi kutoka kwa Allah na mwalimu wa mfumo huu ni Bw. Mtume wetu Muhammad (saw) ambaye kwetu sisi kwake ndio kiogozo kwetu cha kupata jibu sahihi na hiyo ndio njia ya haki, fikira sahihi na ndio mfumo wetu wa maisha.

Kama nilivyotangulia kusema kuwa leo tunatakribani karne moja miaka karibu mia moja tangu iangushwe Dola ya  Kiislamu katika ramani ya dunia.Ama tukirudi kwenye mada ya vyama vingi katika Demokrasia;ambayo leo hii tunaiiishi ndani ya duara na chini ya misingi ya demokrasia .Ama kwa hakika leo tunaishi kwenye kadhia kubwa na msiba endelevu,ukiwemo uchumi,ukabila ukosefu wa ajira na kupanuka pengo la umasikini .Na hii inatokana na mfumo mbaya wakiasilimali  ilio tabikisha  nidhamu mbovu ya demokrasia.Naam katika demokrasia vipi wao walianzisha  vyama vingi.Wasomi wa fikira hii waliutizama mujitamaa  ule mkusanyiko wake wakafahamu kwamba ndani wanadini  tofauti,rai,maslahi na mahitaji ,mazingira ya maisha yao pia ni tofauti, kwa hali hii wakawa ni lazima wawe na vikundi ili waweze kufikia kwenye mahitaji yao na hivi ndivyo vikazuka vyama katika mujtamaa ambavyo mwakilishi ni katika viongozi wa chama ;harakati au mungano na nilazima  vitambuliwe kisiasa na baya zaidi  vyama  hivi vina kubali  dini zote ni sawa mbele ya Allah taala bali  unalazimishwa kukubali  kwamba watu wote wana abudu mungu mmoja na hii ni ajenda mbaya kabisa katika Uislamu;Licha ya kwamba ajenda yao inateganisha  dini na siasa;ambayo siasa ndio njia ya kumleta huyu  mwanadamu imam awe karibu na mola wake  na kupitia siasa anaweza akawa mbali vile vile na mola wake.Hivyo basi wakafunga  milango ya kutosimama chochote juu ya misingi ya dini au kinyume na fikira yao ya kirasilimali.Na hapo ndipo hasa palipozaliwa neno siasa kali,makundi ya kigaidi,sasa hivi uchochezi au msaliti wa Amani.Dira  hino ikaweza kudhibiti  mpanuko wa kifikra kwa umma na hata yale  makundi yanayo  jiita makundi  ya Dini yamejifunga ndani ya  nyororo hino chini ya hifadhi ya  serikali zao za  kitwaghuti.

Enyi watu ,Hakika Democrasia ni mwito mbaya sana mbele ya mwenyezi  mungu kwani unahalalisha yale mwenyezi mungu alioyakataza zamani sana .Takribani miaka 1500 Hijira hadi leo bado  mwanadamu  huyu kishipa amekazana kupigia  debe ushoga  riba na kusagana ;MUNGU  Awalaani wale  wanaoitikadi  kwamba Democrasia  tosha ,bali sisi tunasema uislaamu tosha ; Ama kutokana na matatizo mengi duniani  ni wazi kwamba Democrasia imeshindwa na uongozi jumla sio Ulaya wala America sio  bara Arabu,  India,  uchina wala Africa  kote ni shida  Tupu,imma  vita  vya uchochezi wao,Ama sababisho la umasikini kutoka kwao.Inshallah uislaamu  haujakataza  vyama vingi lakini lazima vijiunge na ageeda yao tutakuja kusoma nakala nyengine .Wabillah taufiq.

No comments: