KWA HABARI NA UCHAMBUZI WA UHAKIKA,KITAIFA NA KIMATAIFA,USIKOSE KUTEMBELEA BLOG HII.

Sunday, August 30, 2015

UCHAGUZI MKUU TANZANIA

UCHAGUZI MKUU  TANZANIA: CCM na UKAWA Timu Mbili Chini Ya Kocha Wao Mmoja MAREKANI.

Mwandishi: Suleiman A Mbarouk

Ni wiki kadhaa sasa tokea maamuzi magumu yafanyike kumpata mgombea wa nafasi ya Uraisi kupitia CCM na CHADEMA (UKAWA).

Wanasiasa , wasomi , wafanyabiashara na raia wa kawaida wameshuhudia wasiyoyatarajia kuibuka kidedea kwa John Pombe Magufuli , msomi na Waziri wa Wizara ya Ujenzi kuwa mgombea wa nafasi ya urais kupitia CCM. Mgombea huyu hajawahi kushika hata nafasi ya mjumbe wa kata wa CCM.

Kwa upande mwengine , Waziri Mkuu wa zamani Edward Lowassa , msomi , mfanyabiashara , mwanasiasa na rafiki mkubwa wa zamani wa Raisi anayemaliza muda wake Jakaya Mrisho Kikwete. Pia Lowassa akiwa ni mwanajeshi aliyewahi kupigana vita vya kumng’oa Iddi Amin Dada wa Uganda mwishoni wa miaka ya 70 ,aliibuka kidedea kuwa mgombea wa Uraisi wa Umoja wa Kutetea katiba ya wananchi –UKAWA kupitia chama cha CHADEMA.

Wengi bado wanashaka ya kulikoni na nini hatima ya Tanzania , nchi inayotawaliwa na CCM chama chenye ukomavu wa hali ya juu chama katika kutatua mifarakano ya ndani na umahiri wa viongozi wake. Je, kuna ufa wa ndani usiozibika ?
Udhaifu wa kuyumba kwa maamuzi ulijitokeza tokea wakati wa mchakato wa rasimu ya katiba mpya. Inasemekana Raisi Kikwete ambaye yeye na chama chake wapo upande wa Amerika alishayabariki maoni ya wananchi yaliyokusanywa na Tume ya Warioba ya serikali tatu ,30 Disemba 2013 katika viwanja vya Karimjee Dar Es Salaam http://mkwinda.blogspot.com/2014/03/.
Kwa mshangao wa wengi akaibeza rasimu hiyo hiyo , kwa kishindo katika ufunguzi wa Bunge la Katiba na kuja na ile iliyopendekezwa na chama chake tawala cha CCM ya kuendelea na mfumo wa muungano wa serikali mbili kwa msisitizo kuwa kati ya watu 351,664 waliotoa maoni ni 47,820 ndiyo waliojadili muundo wa muungano ambao ni sawa na 13.6% tu. Kwa kauli yake hiyo 86.4 % bado wanapenda waendelee na mfumo wa serikali mbili. Katika munasaba wa tukio hilo Kikwete alitoa hadithi yenye fumbo zito inayomuhusu mvuvi na jinni. Alisema “Mvuvi aliokota chupa baharini akidhani ndani yake muna mali. Alipoifunguwa chupa hiyo lilitoka jinni lililomshukuru mvuvi kwa kumfanya kuwa huru. Hata hivyo jinni huyo akamwambia mvuvi kuwa ana njaa kali, na chakula chake ni yeye. Mvuvi alipoona kitisho cha maisha yake akatumia hekma kwa kumwambia jinni, kuwa haamini kwa ukubwa alionao anaweza kuingia chupani ., Jini likaonyesha namna linavyoingia chupani . Kwa hafla, mvuvi akaifunga chupa na kuirembea baharini , kuokoa maisha yake”. Kiuhakiki wa lugha namna mambo yalivyotokea naweza kusema jinni lilikuwa CCM na mvuvi ni Kikwete.

Serikali za Ujerumani na Amerika zikatia shaka jinsi ya rasimu ya katiba ilivyopitishwa kwa nguvu katika Bunge la Katiba bila ya ridhaa ya wajumbe wa bunge hilo chini ya Mwenyekiti wake Samuel Sitta.
www.constitutionnet.org/.../report_on_the_tanzania_draft_constitution_.

Kasoro kubwa mojawapo ya kisiasa iliyojitokeza ndani ya CCM ni katika uteuzi wa mgombea uraisi kwa tiketi ya CCM. Wengi walitarajia wanasiasa waandamizi kama vile Waziri Mkuu Mizengo Pinda, Waziri Mkuu wa zamani Edward Lowassa, Waziri Mkuu wa zamani Fredric Sumaye ,Makamo wa Raisi Dr Bilali, Jaji Augostino Ramadhani , Waziri wa mambo ya Nje Bernard Membe na Waziri Pr. Mark Mwandosya wawe miongoni mwa wateule wa tano bora. Kampeni ya kutafuta wadhamini ya wagombea wote hao inaonyesha kuwa Edward Lowassa ndiye anayekubalika kuliko wagombea wote . Lakini Kamati ya Maadili inayoongozwa na Maraisi wastaafu Ali Hassan Mwinyi na Mkapa wakarudisha majina ya Bernard Membe , Januari Mkamba ,John Magufuli, Asha Rose Migiro na Amina Salum Ali na hatimae John Magufuli kuibuka mgombea wa Uraisi.

Hii ni sababu kubwa iliyomfanya Edward Lowassa, Sumaye na baadhi ya viongozi waandamizi wa serikali na wanachama kadhaa kutoka CCM na kujiunga na UKAWA ambao umepata nguvu katika kinyang’anyiro cha kuingia Ikulu Oktoba 2015.

Kwa maoni yangu, mpambano uliopo ni wa timu mbili ambazo tayari zipo uwanjani chini ya kocha mmoja yaani Amerika kutokana na nukta zifuatazo:

Kwanza: Siasa za kisekula hazina rafiki wala adui wa kudumu bali zina maslahi ya kudumu. Kutokana na CCM na serikali yake kujipamba kwa ufisadi, wizi na rushwa , ni dhahiri sehemu kubwa ya umma lazima ujitenge nayo. Amerika haitopendelea ionekane imeshiriki katika maovu haya yaliyofanywa na vibaraka wake ingawaje nyuma ya pazia imehusika. Na hivi ndivyo ilivyowatelekeza vibaraka wake katika Arab Spring na kujiingiza katika wimbi la mageuzi , kuwaweka madarakani vibaraka wengine . Na huu ndio mchezo aliocheza kumuondoa Lowassa CCM kwa mkono wa Kikwete na kumpeleka UKAWA . Na hivi ndivyo ilivyotumika katika uchaguzi wa 2010, wakati mtu wake Kikwete alipokuwa na upinzani mkubwa ilimtumia mtu wake Lipumba wa CUF ili kura zake ziende kwa JK .Kwa hivyo, yoyote kati ya washindani wawili, Magufuli au Lowassa, atakayeungwa mkono na kushinda , Amerika bado itaendelea kuhodhi siasa za Tanzania. Na Uingereza lazima ikubali matokeo na itabakia kuwa kama fisi kungojea mfupa uanguke ipate sehemu yake , kama inavyofanya katika sehemu kadhaa zinazovamiwa na Amerika kama vile Iraq, Afghanistan nk.

Pili: CHADEMA ambacho ndicho kilichotoa mgombea wa Uraisi kupitia UKAWA kina mahusiano ( bilateral relations ) na chama cha Conservative cha Uingereza Lakini moja ya wafadhili wake wakubwa ni Konrad Adenauer Stiftung/KAS ya Ujerumani ambayo ni chama cha Christian Democrat cha Angela Mikel ambacho kina mahusiano makubwa na Amerika. Aidha, mshirika mkubwa wa UKAWA ni CUF ambacho kiasili kimeundwa na Amerika na viongozi wake wakuu ni vibaraka wa Amerika. Kwa hivyo, maslahi ya Amerika yatahifadhiwa ikiwa kutatokea wimbi la upinzani ndani yake. Na wimbi la viongozi wanaomuunga mkono Lowassa limesheheni CHADEMA kujizatiti zaidi kisiasa.

Na mwisho: Amerika inautangaza uchaguzi wa Tanzania iwe mjadala maalum kiulimwengu . Hili linathibitishwa na kipindi maalum cha “Hard Talk cha Voice of America cha ShakaSsali. Tayari mjadala umeshaanza juu mchakato wa uchaguzi Tanzania na kujenga hoja kwa ushahidi wa vipande vya filamu/clipps kuwa Edward Lowasa anakubalika zaidi.

Source: hizbestafrica.com

Friday, August 14, 2015

KUELEKEA UCHAGUZI MKUU TANZANIA

MGONGANO KATI YA UINGEREZA NA MAREKANI WAZIDI KUPAMBA MOTO
Na Ahmad Ali
Aliyekuwa mwana CCM mkongwe Edward Lowasa ndieatakaepeperusha bendera ya UKAWA kupitia chama cha Chadema katika kinyang’anyiro cha uraisi mwezi wa oktoba2015.
Chama pinzani Chadema kimebariki mapokezi ya Edward Lowasa kutokea CCM na kumpatia fursa ya kugombea uraisi kupitia chama hicho, na hatimae UKAWA kutia saini ya makubaliano hayo. Kejeli na kashfa za ufisadi ambazo upinzani walikuwa wakizitoa dhidi ya Lowasa kumbe ilikuwa ni debe tupu bila ya kuwa na ukweli wowote. Na huu ndio uhalisia wa demokrasia.
Baada ya uteuziwaCCM uliofuatiliziwa na kumpatamgombea uraisi kupitia chama hicho, ambapomatokeo yakeyaliwastaajabisha wengi katika chama tawala pamoja na upinzani,kufuatia John Magufuli kuibuka mshindi wakupeperusha bendera ya CCM katika kinyang’anyiro cha urais mwezioktoba Huku matarajio ya wengi yakidharauliwa na kupuuzwa kwa kiasi kikubwakatika uteuzi huo mpaka kupelekea baadhi ya wanachama wa CCM kurudisha kadi na kujitoa moja kwa moja ndani ya chama. Lowasa na Benard Membendioyaliyokuwa matarajio ya wengi katikamchuano wa kinyang’anyiro cha uraisi kwa kupitia tiketi ya CCM.
Matarajio haya ya wengi chini ya kisingizio cha demokrasia yalimalizwa na kusambaratishwa bila huruma kwa nguvu na mabavu.Wengiwalishindwa kuelewa kwamba ubepari au maslahi ya kiuchumi ndio yanayo kuwa mbele kuliko maslahi ya kisiasa au kidemokrasia. Kipimo cha maamuzi ya kufanya jambo au kuachakufanya ni faida na hasara , hii ni kwa mujibu wa mfumo huu mchafu wa kidemokrasia. Hivyo ni ngumu kusikilizwa maamuzi ya wengi ikiwaitasababisha kupotea kwa maslahi ya mabwana wakubwa wakoloni pamoja na vibaraka wao.
Mtikisiko wa uteuzindani ya CCM ulikuwa ni wa kukata na shoka baina ya kambi mbili. Kambi ya Marekani na kambi ya Mwingireza. Na hizi ndio kambi mbili kuu zinazoikondesha CCM, na huu ndio mpasuko wa kikweli ndani ya CCM.
Na mpaka sasa kambi ya Mwamerika ndio kambi yenyemakali na ndio  iliyoibuka na ushindi ndani ya uteuzihuo na kumuacha Mwingereza kwenye mataa na mipango yake mbadala. Kambi ya Mwamerika imefanikiwa kushinda katika chaguzi hizo licha ya kuwa makusudio yake hayakuwa kwa John Magufuli , lakini imekuwa hivyo kutokana na mipango na mashambulizi makali kutoka kambi ya Mwingereza ambayo ilijipanga kisawasawa kuhakikisha koloni linarudi kwa bwana mkubwa wa asili  Mwingereza, kwani hapo mwanzo lilikuwa mikononi mwake lakini  Mwamerikaakamfanyia mapinduzi ya kisiasa na kulitia mikononi mwake.
Mwingereza ameshindwa kulirudisha koloni lake la asili kwa kumtumia Lowasa ndani ya CCM. Lakini bado hajakata tamaa anajaribu kuitupa tena karata yake hii ndani ya Chadema kwa jahazi la UKAWA kwa kumtumia mtuwake yuleyule Edward Lowasa. Na hii ni kutokana na kuelewa Mwingereza kwambamtuwake huyu anavyokubalika katika jamii, na kuona matarajio ya karibu katika kurejesha koloni lake.
Chadema ambacho ni chama chaMwingereza kimempokea mwanakambi mwenzao Edward Lowasa na kumvisha joho la kugombea urais bila hata ya kuona haya kwa kejeli na kashafa za ufisadi walizokuwa wakimshutumu nazoawali kwa siri na kwa dhahiri. Vinywa vyao vimefyata kabisa ,haya na fedheha zimewafika kwa sababu ya maslahi ya urais 10/2015. Hichi kipimo cha kimaslahi ndicho watakachoendeleanacho mpaka hata itakapo hakikishika ndoto yao ya Urais.
Edward Lowasa aliyekuwa Waziri Mkuu katika serikali ya awamu ya kwanza ya Rais Kikwete , mnamo mwezi februari/2008 alijiuzulu rasmi kwa kulazimishwa kuachia ngazi ya kiti cha uwaziri mkuu kuinusuru serikali ya Kikwete kufuatia kashfa ya sakata la Richmond. Hakika ya mambo ni kwamba huu ulikuwa usaliti wa wazi dhidi ya Lowasa. Nakuanzia hapo karata hii ya mwingereza ilielewa rasmi kwamba imeshasalitiwa dhidi ya mipango ya kuwa raisi katika awamu ijayo. Kutokea hapo na kuendelea mpaka sasa takriban miaka sita Lowasa alikuwa katika maandalizi mazito ya ndani ya chama na nje ya chama kwaajili ya kampeni ya uraisi mwaka wa2015. Sio hali ya kushangaza hata kidogo kuonekana mtu huyu akipendwa na wengi, kwa kuwa ametumia miaka mingi kufanya kampeni tena huku akishirikiana nabaadhiya wakongwe wa chama cha CCM kama vile akina Kingunge nk. Hivyo kama sio kutumika mabavu katika uteuzi uliofanyika ndani ya CCM basi Lowasa leo angekuwa mpeperushaji wa bendera ya CCM katika kuwania uraisi mwezi oktoba2015.
Zimetumika nguvu nyingi mno zilizofuatiliziwa na mikakati ya hali ya juu katika kumtengeneza na kumnadi Lowasa kwa uraisi mwaka 2015 kupitia teketi ya CCM. Lakini kwa bahati mbaya matarajio hayakuwa.
Hatahivyo,Mwingereza hayuko tayari kuona nguvu zake hizi zikipotea bure bila mafanikio yoyote, na badala yake ameamua kuitupa tena uwanjani karata yake hii kupitia chama chake cha kikoloni cha Chadema na hatimae kupeperusha bendera ya UKAWA.
CUF ndani ya ndoa ya UKAWA ni chama kilichosimama kwa ajili ya kuchunga maslahi ya Mwamerika, chama hichi kamakilivy CCM kipo nyuma ya Mwamerika , kikifanya kazi na Chadema bega kwa bega ili kuchunguza mikakati yote ya Mwingereza inayopangwa kupitia Chadema.
Mwamerika anapanga namna ya kulidhibiti koloni lake na huku Mwingereza anapanga namna ya kulirudisha koloni lakelaasili mikononi mwake. Hakika ya mambo ni kwamba huu ni mpambano mkali wa wakisiasa wa kukatana shoka kati ya Marekani Uingereza.
Mazingatio
Wakati haya yote yakijiri Umma wa Kiislamu umejikuta ukiwa mnyonge ukiburuzwa tu huku na kule kana kwamba ni mtoto yatima aliefiwa na babaakabaki mwenye kutanga tanga tu. Umma wa Kiislaamu umebakia kuchezewa shere na kudanganywa kama watoto wadogo. Waliambiwa wapige kura ya maslahi katika chaguzi zilizopita na wakapiga ‘kula’ ya maslahi. Matokeo yake baadhi ya mashekhe binafsi yalivimba matumbo yao kwa maslahi yao binafsi, wakafungua taasisi zao za kibiashara binafs,i na baadhi wamevurumishwa magerezani na wale wale waliowapigia kura hiyo hiyo ya maslahi. 
Kwahivyo,Ummabadoupo katika machungu na maumivu yapo pale pale. Bado haujapata kuona kwa jicho la wazi na kufunguka akili zao ili zipate kuona uharamu na uchafu wa kushiriki michezo hii ya kiulaghai inayofanywa na wamagharibi kupitia kichaka cha demokrasia.
Misibahiinibaada ya kuanguka kwa Dola ya Kiislaam (khilafah Othmaaniyya) tangumwaka 1924 ambapoUmma wa Kiislaamu umezama kwenye shimo lakiza kinene ukakosa wa kuwakinga dhidiya dhiki, dhulma,uonevu na mateso kutoka kwa makafiri na vibaraka wao.
Lakini kwa Waislaamu wenyekujitambua, tunaamini kuwa hali hii inamwisho kwa uwezo waAllah Taala. Kwani kila lililo na mwanzo halikosi mwisho.Namwisho wa dhulma hizi ni pale itakapo rejeatena dola ya Kiislamu ya Khilafa inshallah , kama vile alivyobashiri Rasuli s.a.w kwa kauli yake aliposema: 
“ Kisha itarudi tena khilafah kwa njia ya Utume”

Kutumia Jeshi Kiufisadi Ili Kubaki Kwenye Mamlaka



Na Kassim Agessa

Habari:

Katika gazeti la The Standard la Agosti 1, 2015, Roselyn Obala na Juma Kwayera waliandika kuwa, 'Jukumu la Jeshi la Kenya (KDF) katika usalama wa ndani inaweza kuongezeka kama mapendekezo katika mswada mpya yatakuwa sheria.

Mswada wa Marekebisho ya KDF 2015, ikipitishwa kuwa sheria, itampa mamlaka Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi kupeleka KDF katika shughuli za kiraia. Hoja hi kwa kiasi kikubwa ni mabadiliko ya uendeshaji na amri iliyo kwa sasa mikononi mwa Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP). Vile vile, Katibu wa ulinzi katika baraza la Mawaziri hana jukumu kubwa katika kukabidhi majukumu ya kiraia kwa Mkuu wa Majeshi. Mswada huu ulioko katika hatua ya uchapishaji ina ishara ya muundo wa vikosi vya usalama katika Uganda, Rwanda, Ethiopia na Sudan, ambapo hakuna mpaka wazi katika upeo wa kazi za polisi na jeshi. Nchini Uganda na Ethiopia, kwa mfano, Jeshi ndio hutumika wakati wa uchaguzi kusimamia vituo vya kupigia kura.

Maoni:

Ingawa mswada wenyewe bado haujawekwa nje kwa uchunguzi, nia yake ni wazi kabisa. Kwa kuutazama mswada huu kwa haraka haraka unadhihirisha kuwa mapendekezo hayana ubaya wowote zaidi ya serikali kuhuisha shughuli za huduma zake za usalama ili kukabiliana na vitisho vya usalama. Hata hivyo, sababu za kimsingi zinaonyesha kuwa mswada huu hauna uhusiano wowote na kulinda nchi badala yake ni kuimarisha nguvu na kujenga vipenyezo  vya ufisadi mbali kabisa na macho ya ummah. Makala ya The Standard yanaendelea kueleza kuwa Mswada pia unalenga kuanzishwa kwa kikosi maalum cha akiba kinachojumuisha Huduma ya Kulinda Wanyamapori (KWS), Walinzi wa Misitu (KFS) na Huduma ya Vijana kwa Taifa (NYS) kutumikia pamoja na KDF. "Rais anaweza katika hali ya dharura au maafa au wakati wa vita, au machafuko kuamrisha kikosi hiki cha Walinzi wa Misitu na NYS kuajiriwa kutumika pamoja na KDF au vinginevyo katika ulinzi wa taifa ima ndani au nje ya nchi". Viongozi wa CORD hivi karibuni wametuhumu utawala wa Jubilee kwa madai ya kujaribu kuiaanda NYS kijeshi lakini wakapuuzwa kwa kudaiwa kuwa na wivu kwa kazi nzuri vijana walikuwa wakifanya katika vitongoji duni! Ni kawaida viongozi kuunda wanamgambo kwa jina la vijana wa chama au kwa swala hili, kusingizia kuwawezesha vijana ambao wanaweza kutumika kwa haraka kusababisha vurugu. Maandamano mjini Nairobi mnamo Juni 22 na vijana kuunga mkono miradi ya NYS na maandamano pinzani yaliyofuatia mnamo Juni 23 katika mitaa ya Kibera dhidi ya miradi hiyo ni utangulizi wa kile tunatarajia kuwa mwanzo wa mbinu hii.

Mswada huu unampa Rais uwezo wa kuongeza mda wa kuhudumu kwa ofisi Mkuu, Makamu Mkuu na Makamanda wa KDF kwa kipindi kisichozidi mwaka mmoja na pia inataka kupanua umri wa kustaafu wa Mkuu wa KDF kutoka miaka 62 hadi 64. Hii ni kimsingi kiashiria kwamba usalama wa Nchi unategemea watu binafsi badala ya taasisi. Jambo ambalo lapelekea mda wa kuhudumu kuongezwa kwa vile hakuna warithi. Jakoyo Midiwo, Mbunge wa Gem alinukuliwa akisema "Serikali inajenga nafasi ya Usalama wa Nchi kupitia mlango wa nyuma ili kurudisha kazini Mkuu wa Jeshi aliyestaafu Julius Karangi. Hii haikubaliki" na kushutumu serikali kujaribu kuanzisha serikali ya kijeshi. Katika kipindi cha NTV cha Watu na Siasa kilichopeperushwa hewani Agosti 10, 2015, wazungumzaji walielezea kuhusu serikali ya Uhuru kwa taratibu kugeuzwa kijeshi kwa kutarajia uwezekano wa kuanzisha mabadiliko ya muhula wa Rais ambao kiwango chake ni vipindi viwili vya miaka mitano. Huu umekuwa mtindo na Marais wa kiafrika kukimbilia kubadili sheria kwa ajili ya kuruhusu utawala bila kiwango cha mda kuwekwa na Burundi, Rwanda na Uganda ni mfano mzuri. Jeshi ama wanamgambo  wanalengwa kutumika hapa ikiwa raia hawataki kufuata matakwa ya walio mamlakani.

Mswada huu pia unaondoa sharti la KDF kutangaza nafasi kwa mujibu wa majimbo. Nia ya kifungu hiki ni wazi kwa watu wote kwamba kinajaribu kuhakikisha kuwa wengi wa walio katika jeshi wanatoka maeneo ya Rais. Wanatarajiwa kutegemewa kwa kutumiwa ikiwa hali itajitokeza ambapo uongozi wa aliye kwenye mamlaka unapata tishio kutoka kwa wapinzani. Pia unakinga shughuli za KDF, ikiwa ni pamoja na matumizi ya bajeti yake na kazi yake kutokana na uchunguzi wa umma kwa kunyima Bunge jukumu la uhasibu. Ingawa bunge pia ni pango la rushwa na kwa hivyo si taasisi ya kuthaminiwa kufanya uhasibu, inatarajiwa kwamba uchunguzi wa umma kuhusu matumizi ya KDF ni muhimu sana ikizingatiwa wao ni walipa kodi. Waandaalizi wa mswada huu ni wazi nia yao ni kujificha nyuma ya pazia la 'Kandarasi za Kiusalama' ili kuficha njama zao.

Kutokana na uchambuzi juu ya matukio yanayozunguka mapendekezo ya mswada huu, inaweza kuonekana kwamba usalama na rushwa waenda sambamba katika nchi za Kibepari. Na haijawahi kuwa lengo ni kuhifadhi nchi badala yake ni kuhifadhi maslahi ya pamoja ya tabaka la wanasiasa na mabwenyenye. Utawala huu umejifunza kwa haraka kutoka kwa mabwana zake katika nchi za Magharibi kwamba serikali kufanikiwa ni lazima kubuni migogoro na kisha kusingizia baadae uwezo wa kutatua. Baada ya kukosea katika kila operesheni ya usalama iliyofanywa tangu operesheni 'Linda Nchi', serikali ilianza safari ya kujenga hali ya kudumu katika mizozo katika mabongo ya wananchi kwa matumaini kwamba wataunga mkono miswada kama hii ambayo kiujanja ina lengo la kuwanyamazisha. Ni wazi kuwa Serikali imeshindwa na jukumu lake la kutoa ulinzi kwa wananchi wake kutokana na kushindwa kubadilisha kimuundo vyombo vya usalama. Kwa bahati mbaya, hii inaonekana kufanywa kimakusudi kwa vile Shilingi billion 74 zilizotengwa katika bajeti kwa ajili ya jeshi ni kivutio kikubwa kwa magenge ya ufisadi.

Kwa kumalizia, Uislamu hautoi mda kwa Khalifa kuhudumu na kukaa kwake katika mamlaka haihusiana na kuungwa mkono na jeshi lakini kwa kuzingatia shariah. Kupitia thakafa ya kina kwa raia, serikali ya Kiislamu huhakikisha kwamba kila mmoja anaelewa jukumu lake katika jamii. Ni hofu ya kuhisabiwa na Muumba na ummah kwa ujumla ndio inafanya viongozi katika serikali ya Kiislamu kupeleka mambo yao kwa manufaa ya ummah. Kwa kuwa hakuna serikali ya Kiislamu, ni wajibu juu ya umma kuwa macho dhidhi ya njama za serikali hizi za kikafiri ambazo hutunga sheria zinazoweza kuzuia kusimamishwa kwa serikali ya Khilafah.

CHIMBUKO LA VYAMA VINGI NDANI YA MFUMO WA KIDEMOKRASIA

CHIMBUKO LA VYAMA VINGI NDANI YA MFUMO WA KIDEMOKRASIA

Na Farijala malid

Bismillah-Ar-rahaman

Kikawaida kwa kila zama,fikira katika ulimwengu ina chimbuko lake  ima chimbuko  hilo litoke kwa mwenyezi mungu  au kwa mwanadamu.Takribani miaka 100;{karne moja} katika umma huu waliishi nje ya fikira ambayo chimbiko lake ni Mwenyezi Mungu yaani mfumo wa Uislam ambao umeletwa kwa njia ya wahyi kutoka kwa Allah na mwalimu wa mfumo huu ni Bw. Mtume wetu Muhammad (saw) ambaye kwetu sisi kwake ndio kiogozo kwetu cha kupata jibu sahihi na hiyo ndio njia ya haki, fikira sahihi na ndio mfumo wetu wa maisha.

Kama nilivyotangulia kusema kuwa leo tunatakribani karne moja miaka karibu mia moja tangu iangushwe Dola ya  Kiislamu katika ramani ya dunia.Ama tukirudi kwenye mada ya vyama vingi katika Demokrasia;ambayo leo hii tunaiiishi ndani ya duara na chini ya misingi ya demokrasia .Ama kwa hakika leo tunaishi kwenye kadhia kubwa na msiba endelevu,ukiwemo uchumi,ukabila ukosefu wa ajira na kupanuka pengo la umasikini .Na hii inatokana na mfumo mbaya wakiasilimali  ilio tabikisha  nidhamu mbovu ya demokrasia.Naam katika demokrasia vipi wao walianzisha  vyama vingi.Wasomi wa fikira hii waliutizama mujitamaa  ule mkusanyiko wake wakafahamu kwamba ndani wanadini  tofauti,rai,maslahi na mahitaji ,mazingira ya maisha yao pia ni tofauti, kwa hali hii wakawa ni lazima wawe na vikundi ili waweze kufikia kwenye mahitaji yao na hivi ndivyo vikazuka vyama katika mujtamaa ambavyo mwakilishi ni katika viongozi wa chama ;harakati au mungano na nilazima  vitambuliwe kisiasa na baya zaidi  vyama  hivi vina kubali  dini zote ni sawa mbele ya Allah taala bali  unalazimishwa kukubali  kwamba watu wote wana abudu mungu mmoja na hii ni ajenda mbaya kabisa katika Uislamu;Licha ya kwamba ajenda yao inateganisha  dini na siasa;ambayo siasa ndio njia ya kumleta huyu  mwanadamu imam awe karibu na mola wake  na kupitia siasa anaweza akawa mbali vile vile na mola wake.Hivyo basi wakafunga  milango ya kutosimama chochote juu ya misingi ya dini au kinyume na fikira yao ya kirasilimali.Na hapo ndipo hasa palipozaliwa neno siasa kali,makundi ya kigaidi,sasa hivi uchochezi au msaliti wa Amani.Dira  hino ikaweza kudhibiti  mpanuko wa kifikra kwa umma na hata yale  makundi yanayo  jiita makundi  ya Dini yamejifunga ndani ya  nyororo hino chini ya hifadhi ya  serikali zao za  kitwaghuti.

Enyi watu ,Hakika Democrasia ni mwito mbaya sana mbele ya mwenyezi  mungu kwani unahalalisha yale mwenyezi mungu alioyakataza zamani sana .Takribani miaka 1500 Hijira hadi leo bado  mwanadamu  huyu kishipa amekazana kupigia  debe ushoga  riba na kusagana ;MUNGU  Awalaani wale  wanaoitikadi  kwamba Democrasia  tosha ,bali sisi tunasema uislaamu tosha ; Ama kutokana na matatizo mengi duniani  ni wazi kwamba Democrasia imeshindwa na uongozi jumla sio Ulaya wala America sio  bara Arabu,  India,  uchina wala Africa  kote ni shida  Tupu,imma  vita  vya uchochezi wao,Ama sababisho la umasikini kutoka kwao.Inshallah uislaamu  haujakataza  vyama vingi lakini lazima vijiunge na ageeda yao tutakuja kusoma nakala nyengine .Wabillah taufiq.