KWA HABARI NA UCHAMBUZI WA UHAKIKA,KITAIFA NA KIMATAIFA,USIKOSE KUTEMBELEA BLOG HII.

Sunday, December 13, 2015

SHEREHE ZA JAMHURI KENYA NA UHURU WA BENDERA.




Kila mwaka ifikapo mwezi wa disemba tarehe 12,huwa ni siku kuu ya kitaifa nchini Kenya.Siku hio huwa ni kwa minajili ya kuadhimisha siku Kenya ilipokuwa ikingia rasmi kwenye dira ya mfumo wa kikoloni ubepari democrazy, kwa njia ya jamhuri(republicanism).
Jamhuri huwa ni mfumo wa kiutawala wa kibepari wenye kudhamini nyadhifa za serikali kuwa wazi na kugombewa kwa njia ya kura kila baada ya muhula fulani,ikiwa moja ya njia ya kustiri hali ya mfumo wao muovu na pia kumdumisha yule atakae kuibuka mtwiifu kwao kama Yoweri Kaguta Museveni.Licha kuwa mtawala wa kiimlaa kuwakandamiza wapinzani na upinzani wa vyama vingi unao lazimishwa kwengine yeye hana wala hapigwi vita.

Kufuatilia mkutano wa Berlin Conference ulioandaliwa na wakoloni kujigawia ngawira za rasilimali za madola mengine ukiongozwa na Chancellor Otto von Bismarck wa Ujerumani,Kenya iliitwa British East Africa,na kupewa Waingereza kuitawala ambae akaleta walowezi(settlers) wa kizungu kuja kutwaa mashamba ya wenyeji wa Kenya.

Licha ya idadi yao ndogo walowezi hao walikuwa na ushawishi na msemo ktk serikali yao ugenini Kenya.
Huku wenyeji wenye asili ya kiafrika na wahindi,wakiwa hawana hawanani bali hata ardhi zao ziliporwa na wakatimuliwa kama Waislam wanavyofanywa leo Falastin na mayhudi, kubwa isitoshe wenyeji walikuwa wakitozwa ushuru kufanyishwa kazi za sulubu na kulipwa mshahara duni.

Baada ya wakoloni kuchoshwa na sera zao za kuwasimamia wengine moja kwa moja(direct rule),walichochea fikra za uhuru kwa kuamsha hisia za uzalendo na utaifa miongoni mwa wenyeji na walipoweza hata hisia mbovu za ukabila.
Japo raia wa kawaida walihadaiwa ati wapigana na wakoloni ili kuwatimua na kurudisha rasilimali mikononi mwao.
Ukweli ni kuwa wakoloni hawakushindwa kivita wala jambo hili haliingii akilini. Waafrika,wahindi na waarabu walokuwa na silaha duni hafifu zama zile,waweze kushinda jeshi la serikali kuu au wakoloni waliokuwa na ndege ,manuwari,vifaru,bunduki na hata kushiriki vita vikuu duniani.

Ukweli ni kuwa wakoloni walibadilisha sura mpya ya ukoloni,Kutoka ile ya zamani ilokuwa ikitoa hali ya dhati kamili ya uovu wa mfumo wao kutoka kwa wakoloni moja kwa moja hadi hini ya sasa,ambapo nchi hupachikwa vibaraka wenye kuwahudumia wazungu.

Na mapungufu ya mfumo huo yamesitirika kiasi kwani huonekana kama dosari ya viongozi vyama tawala au miuungano ya kisiasa.
Wala sio wakoloni na mfumo wao duni kama ilivyo hali kwa sasa.
Kila mfumo ukionyesha kucha zake mbovubasi viongozi hasa wa upinzani au raia adi wasojua dhati na uhalisia wa mfumo huo hudai kuwa viongozi waliomamlakani,ndio waovu.
Wapinzani huzidisha kutia chumvi ili kutafuta kula huku raia wakitumiwa kama ngazi.
Tujiulize kama si mfumo kuwa ndio shina la matatizo mbona America ishabadili marais na ishapiga kura zaidi ya miaka 200,hadi sasa kuma dosari na mapungufu mengi.
Na kila mgombezi adai sawa wa upinzani au utawala,wadai kuleta islahi na kuondoa shida.

Sera hii mpya ya ukoloni ilimpa Jomo Kenyatta,urais wa kwanza nchini 12:12:1963.Hili halikutokea rahisi bali baada ya kumpika kwa miaka na dahari ktk safari zake za Uingereza.

Hapa Jomo Kenyatta aliibuka kufaa zaidi hivyo ikabidi wamlinde kwa miaka takriban 7 kwa kumueka jela kwa kisingizio ati ni mpinzani wao mbaya,Mau Mau hatari na tishio kwa usalama.
Japo Percy Sillitoe,aliekuwa mkurugenzi mkuu wa majasusi wa M15 wa Uingereza zama zile alithibitisha kuwa madai haya ni uongo wala hayana ukweli.Ktk barua aliomuandikia gavana wa Kenya,Evelyn Baring tarehe 9:1:1953 alisema,
"Our sources have produced nothing to indicate that Kenyatta or his associates in the UK are directly involved in Mau Mau activities or that Kenyatta is essential to Mau Mau as a leader or that he is in a position to direct activities!"
(Source;Andrew pg 454)

Kufuatia amri na msukumo wa serikali yake ya Uk,Evelyn Baring aliendelea na kutangaza hali ya hatari 21:10:1952,na kuanzia kuwashika na kuwatesa wapinzani wa ukoloni na vibaraka.

Na kuwaeka ktk hali duni mbaya isio ya kibinadamu kufikia hadi kamishna wa polisi wa kikoloni Arthur Young,akamuandikia gavana wa Kenya zama zile Evelyn Baring barua mnamo 22:11:1954 akilalamika,
"The horror of some of the so-called Screening Camps now present a state of affairs so deplorable that they should be investigated without delay,so that the ever increasing allegations of inhumanity and disregard of the rights of the African citizen are dealt with and so that the government will have no reason to be ashamed of the acts which are done in its own name by its own servants."
(Source; Taking on The Boss:The Quiet Whistle Blowers on Events In Kenya Deserve Praise).

Kufuatia kusalitiwa na jamaa zao wenyewe,Mau Mau walitoa vitisho kwa Jomo Kenyatta, kutaka kumuua kwa kushirikiana na wakoloni kama alivyodhihirisha mwenyewe Kenyatta ktk hotuba yake April 1963,

"We are determined to have independence in PEACE,and we shall not allow HOOLIGANS to rule Kenya.
We must have no hatred towards one another .Mau Mau was a DISEASE which had been eradicated and must NEVER BE REMEMBERED again! (Source Clough 1998 p25).

Hivyo kupelekea kushikwa kwa hasimu na mpinzani wake mkuu, aliekuwa adui mkubwa wa wakoloni Dedan Kimathi,20:10:1956, hatimae kumuua kwa kumnyonga si yeye tu bali kila alojitolea muhanga kuwapinga na kupigana kidhati dhidi ya wakoloni na vibaraka(loyalists) wao ambao walituzwa kwa nyadhifa tofauti ktk serikali kuanzia pamoja na kugawiwa ardhi kubwa kama zawadi.

Jumamosi tarehe 12:12:2015,Kenya imesherehekea tena sherehe za jamhuri ikiwa ni za 52 tangu Kenya kutangazwa kuwa jamhuri 12:12:1964.Au kama raia wanavyohadaiwa na wakoloni na vibaraka wao.
Licha ya kuwa Kenya kuna kiongozi mmoja,bendera moja,wimbo wa taifa mmoja,court of arms moja,zote zikiashiria UMOJA.
Ukweli ni kuwa nchi imegawanyika tena vibaya Kwa misingi ya kimajimbo,maeneo,kikabila.Ili mtu awe rais Kenya,lazima awe na ushawishi mkubwa wa kabila lake bali kufaulu ni awe kiongozi wa kabila lake kamwe si ktk serikali wala upinzani.

Gonjwa hili lipo na tiba yake pekee ipo kwenye Uislam kama mfumo kamili wa maisha chini ya kivuli cha Khilafah.
Kwa sababu kivitendo Uislam ushalitokomeza kama bado Waislam wangali nalo ni matunda ya kutawaliwa na mfumo wa kikoloni ubepari democrazy.

DAWAH NI QAUL NA AMAL

No comments: