Vita vikali vya kielektroniki dhidi ya Hizb ut Tahrir Na hatimaye kufungwa kwa Ukurasa wa Facebook wa Ameer wa Hizb ut Tahrir
Ijumaa, Des 04 2015 Kwa Vyombo Vya Habari
(Tafsir)
Tangu kutokea msururu wa visa vya mashambulizi ya kupangwa, vilivyojumuisha ushambuliaji wa risasi, kutekwa nyara mateka, katika Jiji la Paris nchini Ufaransa siku ya Ijumaa jioni, Novemba 13, 2015, njama za kiulimwengu zilitangazwa kupambana na tovuti za ISIS. Ajabu ilijumuisha na tovuti rasmi ya harakati ya Hizb ut Tahrir, chama cha kisiasa cha Kiislam ambacho hakitumii mabavu katika njia iliojifunga nayo, kufikia malengo yake, kwani haya yakiuka taratibu za Kisharia za kuleta mageuzi. Juu ya haya, tovuti yake ilijumuishwa miongoni mwa zile zenye kulengwa, licha kuwa Hizb ut Tahrir imekariri mara kadha katika matukio tofauti kuwa yapinga njia inayofuatwa na ISIS, na kuwa haina mafungamano ya ndewe wala sikio na ISIS. Lakini miungano na serikali zenye uadui dhidi ya Hizb ut Tahrir, hilo halikuwa pingamizi kwao kutofunga tovuti zake, dhihirisho la uadui na uhasama dhidi ya Uislamu na Waislamu.
Jana Jumanne, 01/12/2015 saa 4:00 pm, usimamizi wa Facebook ulijitwika jukumu la kuondoa ukurasa wa mwanachuoni mkuu Sheikh Ata Bin Khalil Abu al-Rashtah, Ameer wa Hizb ut Tahrir, na kumfungia licha kuwa,ukurasa huo ulikuwa na nishati na wapendwa sana.Ulikuwa ukijadili matukio ya kila siku katika kila nyanja za kimaisha ima Kisiasa, Kifikra na Kithaqafa, Kifiqhi akijibu masuali kadha aliyotumiwa Ameer wa Hizb, huku Ummah ukimuamini, kielimu na kiufahamu wake wa kina alionao juu ya masuala tofauti.Kukiwa na watu wengi wenye kuipenda, kushirikiana na kutoa maoni yao tofauti tofauti huku idadi ya wanaoshiriki katika ukurasa wake ukizidi idadi ya watu 263,500. Jambo hili, likawakosesha lepe madhalimu na kuwapelekea kunoa ndimi zao za chuki na uhasama dhidi ya Uislamu na Waislamu hasa wabebaji wa ulinganizi wa Uislamu kwa usafi wake. Hivyo wakaanza kampeni kali dhidi ya ukurasa huo, kwa siku kumi kufuatana bila kuchoka.
Kando na kutuma barua kwa wasimamizi wa Facebook kuwasihi wasiufunge ukurasa huo, na kuwajulisha kuwa hatujapokea sababu yoyote ya kimsingi ya kuufunga ukurasa huo. Ajabu wasimamizi wa wa Facebook hawakujibu barua hiyo, badala yake wakasisitiza kuufunga ukurasa! Hili ladhihirisha kuwa ufungaji huu, ulifanywa kiuadui, bila kuwepo sababu yoyote muafaka, bali chuki dhidi ya Uislamu na Waislamu.
Kufungwa kwa ukurasa huo, wenye ucha Mungu na mafunzo ya hekima, ni moja wapo ya vita vya makufar vya msalaba dhidi ya Uislamu na Waislamu, kwa sababu yakuueleza Uislam kwa usafi wake, kama ulivyo teremshwa na Ar Rasul Muhammad (saw), na mtazamo safi na haki wa kisiasa ,unawafanya Waislamu kumtambua ndugu yao wa dhati mwenye kujitolea kuwahudumia licha ya kuviziwa na adui.
Daima dawama Kaffir wa kimagharibi, ana upangia njama ulinganizi safi wa Kiislamu, akidhani kwa kufanya hivyo atazuia nuru yake au, kuwaficha watu ukweli wake.Haya ni matokeo ya kupata hali ngumu na kukosa usingizi kwa ujumbe mzito wa harakati.Hivyo ikaamua kutumia silaha zake zote, kutumia uamuzi wa kikoloni uliopo mabongoni mwao,na kuwamrisha vibaraka wake wote na mamluki wake kuupiga vita Uislamu na Waislamu. Hata neno la kweli dogo kwao limekuwa tishio kubwa, likiwatia hofu na kuwa nyima usingizi.Hivyo wanawaamrisha majasusi wao wote,njama hizi mbovu, hatimaye kutumia uadui wao na chuki kufunga ukurasa huo mwema katika vita vya msalaba dhidi ya Uislamu na Waislamu.Lakini haya yote ni bure.Wala hawataweza kuizima Nuru ya Allah!
يُرِيدُونَ أَن يُطْفِؤُواْ نُورَ اللَّهِ بِأَفْوَاهِهِمْ وَيَأْبَى اللَّهُ إِلاَّ أَن يُتِمَّ نُورَهُ وَلَوْ كَرِهَ الْكَافِرُونَ * هُوَ الَّذِي أَرْسَلَ رَسُولَهُ بِالْهُدَى وَدِينِ الْحَقِّ لِيُظْهِرَهُ عَلَى الدِّينِ كُلِّهِ وَلَوْ كَرِهَ الْمُشْرِكُونَ
“Wataka kuizima Nuru Ya Allah kwa midomo yao,lakin Allah Akataa ila kuitimiza Nuru Yake hata kama makafir wachukia.Yeye Ndie Aliemtuma Mtume Wake na Uongofu na Dini Ya haki, ili idhihiri juu ya dini zote japo makafiri wachukia.”[At-Tawba: 32-33]
Toleo No: 1437 AH /010 Wednesday, 20th Safar 1437 AH 02/12/2015 CE
No comments:
Post a Comment