Vita vikali vya kielektroniki dhidi ya Hizb ut Tahrir Na hatimaye kufungwa kwa Ukurasa wa Facebook wa Ameer wa Hizb ut Tahrir
Ijumaa, Des 04 2015 Kwa Vyombo Vya Habari
(Tafsir)
Tangu kutokea msururu wa visa vya mashambulizi ya kupangwa,
vilivyojumuisha ushambuliaji wa risasi, kutekwa nyara mateka, katika
Jiji la Paris nchini Ufaransa siku ya Ijumaa jioni, Novemba 13, 2015,
njama za kiulimwengu zilitangazwa kupambana na tovuti za ISIS. Ajabu
ilijumuisha na tovuti rasmi ya harakati ya Hizb ut Tahrir, chama cha
kisiasa cha Kiislam ambacho hakitumii mabavu katika njia iliojifunga
nayo, kufikia malengo yake, kwani haya yakiuka taratibu za Kisharia za
kuleta mageuzi. Juu ya haya, tovuti yake ilijumuishwa miongoni mwa zile
zenye kulengwa, licha kuwa Hizb ut Tahrir imekariri mara kadha katika
matukio tofauti kuwa yapinga njia inayofuatwa na ISIS, na kuwa haina
mafungamano ya ndewe wala sikio na ISIS. Lakini miungano na serikali
zenye uadui dhidi ya Hizb ut Tahrir, hilo halikuwa pingamizi kwao
kutofunga tovuti zake, dhihirisho la uadui na uhasama dhidi ya Uislamu
na Waislamu.
Jana Jumanne, 01/12/2015 saa 4:00 pm, usimamizi wa
Facebook ulijitwika jukumu la kuondoa ukurasa wa mwanachuoni mkuu Sheikh
Ata Bin Khalil Abu al-Rashtah, Ameer wa Hizb ut Tahrir, na kumfungia
licha kuwa,ukurasa huo ulikuwa na nishati na wapendwa sana.Ulikuwa
ukijadili matukio ya kila siku katika kila nyanja za kimaisha ima
Kisiasa, Kifikra na Kithaqafa, Kifiqhi akijibu masuali kadha aliyotumiwa
Ameer wa Hizb, huku Ummah ukimuamini, kielimu na kiufahamu wake wa kina
alionao juu ya masuala tofauti.Kukiwa na watu wengi wenye kuipenda,
kushirikiana na kutoa maoni yao tofauti tofauti huku idadi ya
wanaoshiriki katika ukurasa wake ukizidi idadi ya watu 263,500. Jambo
hili, likawakosesha lepe madhalimu na kuwapelekea kunoa ndimi zao za
chuki na uhasama dhidi ya Uislamu na Waislamu hasa wabebaji wa
ulinganizi wa Uislamu kwa usafi wake. Hivyo wakaanza kampeni kali dhidi
ya ukurasa huo, kwa siku kumi kufuatana bila kuchoka.
Kando na
kutuma barua kwa wasimamizi wa Facebook kuwasihi wasiufunge ukurasa huo,
na kuwajulisha kuwa hatujapokea sababu yoyote ya kimsingi ya kuufunga
ukurasa huo. Ajabu wasimamizi wa wa Facebook hawakujibu barua hiyo,
badala yake wakasisitiza kuufunga ukurasa! Hili ladhihirisha kuwa
ufungaji huu, ulifanywa kiuadui, bila kuwepo sababu yoyote muafaka, bali
chuki dhidi ya Uislamu na Waislamu.
Kufungwa kwa ukurasa huo,
wenye ucha Mungu na mafunzo ya hekima, ni moja wapo ya vita vya makufar
vya msalaba dhidi ya Uislamu na Waislamu, kwa sababu yakuueleza Uislam
kwa usafi wake, kama ulivyo teremshwa na Ar Rasul Muhammad (saw), na
mtazamo safi na haki wa kisiasa ,unawafanya Waislamu kumtambua ndugu yao
wa dhati mwenye kujitolea kuwahudumia licha ya kuviziwa na adui.
Daima dawama Kaffir wa kimagharibi, ana upangia njama ulinganizi safi
wa Kiislamu, akidhani kwa kufanya hivyo atazuia nuru yake au, kuwaficha
watu ukweli wake.Haya ni matokeo ya kupata hali ngumu na kukosa usingizi
kwa ujumbe mzito wa harakati.Hivyo ikaamua kutumia silaha zake zote,
kutumia uamuzi wa kikoloni uliopo mabongoni mwao,na kuwamrisha vibaraka
wake wote na mamluki wake kuupiga vita Uislamu na Waislamu. Hata neno la
kweli dogo kwao limekuwa tishio kubwa, likiwatia hofu na kuwa nyima
usingizi.Hivyo wanawaamrisha majasusi wao wote,njama hizi mbovu,
hatimaye kutumia uadui wao na chuki kufunga ukurasa huo mwema katika
vita vya msalaba dhidi ya Uislamu na Waislamu.Lakini haya yote ni
bure.Wala hawataweza kuizima Nuru ya Allah!
يُرِيدُونَ أَن
يُطْفِؤُواْ نُورَ اللَّهِ بِأَفْوَاهِهِمْ وَيَأْبَى اللَّهُ إِلاَّ أَن
يُتِمَّ نُورَهُ وَلَوْ كَرِهَ الْكَافِرُونَ * هُوَ الَّذِي أَرْسَلَ
رَسُولَهُ بِالْهُدَى وَدِينِ الْحَقِّ لِيُظْهِرَهُ عَلَى الدِّينِ
كُلِّهِ وَلَوْ كَرِهَ الْمُشْرِكُونَ
“Wataka kuizima Nuru Ya
Allah kwa midomo yao,lakin Allah Akataa ila kuitimiza Nuru Yake hata
kama makafir wachukia.Yeye Ndie Aliemtuma Mtume Wake na Uongofu na Dini
Ya haki, ili idhihiri juu ya dini zote japo makafiri
wachukia.”[At-Tawba: 32-33]
Toleo No: 1437 AH /010 Wednesday, 20th Safar 1437 AH 02/12/2015 CE